VIJANA WAASWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UONGOZI CCM TANGA



NA  BONIFACE  GIDEON,  TANGA

Vijana  wametakiwa kujitokeza  kwa wingi  kuchukua  fomu ili  wapate nafasi ya  kugombea  nafasi  mbalimbali za  uongozi  ndani  ya  chama  cha  mapinduzi ccm.

Wito huo  umetolewa  na  katibu mwenezi  wa  chama  cha  mapinduzi ccm  wilaya  ya  Tanga  Lupasio  Kapange wakati  akizungumza  na  waandishi wa  habari  jana, Kapange alisema vijana  ndio  tegemeo  kubwa  ndani  ya  ccm  hivyo  wasiwe  na  woga kuchukua fomu  za kuwania  nyadhifa  mbalimbali  ndani  ya  chama  hicho tawala.

Aliongeza  kuwa  ccm  wilaya ya  tanga  imeshaanza  kutoa  fomu kuanzia  ngazi  ya  kata , matawi na mashina na  tayari wanachama  wameshaanza  kujitokeza  kuchukua  fomu hivyo  ni  vyema  vijana  wakajitokeza  kwa  wingi  kuchukua fomu ''Mchakato  wa  uchaguzi  ndani ya  chama  wilaya  ya  tanga unaendelea  vyema  tupo  katika hatua  ya  utoaji  fomu ngazi  ya kata ,matawi  na  mashina tunawaomba  vijana  kujitokeza  kwa  wingi  maana  wao  ndio  nguzo  ya  ccm, nafasi  zipo  nyingi Kuanzia mashina mpaka  taifa  pia vijana  watambue  kuwa  hakuna gharama  yoyote'' Aliongeza Kapange 

Aidha  akizungumzia mchakato wa  uchaguzi wa chama  cha mapinduzi  wilaya ya Tanga, Kapange  alisema mpaka  sasa  wameshatoa  fomu  kwenye  kata  zote na  mabalozi, aliongeza  kuwa hatua  inayofua  baada  ya hapo nikufanya  uhakiki.

Alisema  ccm wilaya  ya Tanga  imejipanga kuhakikisha inasimamia mchakato  wa uchaguzi  na  hakuna  mwanachama yeyote mwenye  sifa zinazokidhi  vigezo  vya uongozi  atakayeonewa ,  aliwataka wanachama wanaochukua fomu za kuwania  nafasi  za  uongozi kuepuka  kutoa  au kupokea   Rushwa  kwani wakigundulika  hawatapata  nafasi  za uongozi  ndani ya  ccm.

Maoni