Kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Benedict Wakulyamba akizungumza na Waandishi wa habari( picha na Boniface Gideon )
NA BONIFACE GIDEON, TANGA
Jeshi la police hapa mkoani Tanga kwakushirikiana na kikosi cha usalama barabarani limefanikiwa kukamata zaidi ya pikipiki 225 kutokana na makosa mbalimbali ya usalama barabarani.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Benedict Wakulyamba alisema operesheni hiyo ya kukamata pikipiki zinazojihusisha na Uhalifu wa barabarani pamoja na makosa ya usalama barabarani ulianza Tar. 22 April na ilihusisha wilaya zote za mkoa wa Tanga.
Aliyataja makosa yaliyo sababisha kukamatwa kwa pikipiki katika operesheni hiyo kuwa nipamoja na Ubovu wa pikipiki -50 , makosa ya kuvaa kofia ( Helmenti ) walikamata pikipiki 58 , makosa ya kutokuwa na Bima walikamata pikipiki 42 , makosa ya kuzidisha Abiria walikamata pikipiki 01 , makosa ya kuendesha pikipiki bila leseni ( D/LICENCE ) Walikamata pikipiki 74.
Kamanda Wakulyamba alibainisha kuwa mara baada ya kukamata pikipiki hizo waliweza kuchukua hatua mbalimbali kutokana na aina ya makosa alizitaja baadhi ya hatua zilizochukuliwa kuwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa 19 , kuwalipisha faini watuhumiwa 15 ambapo waliweza kupata zaidi ya TSH.450,000/= aliongeza kuwa makosa ya kutokulipa kodi TRA yapo 33 na tayari yashughulikiwa na mamlaka ya mapato TRA Mkoa wa Tanga, alisema pikipiki zilizoachiwa 18 huku pikipiki 184 zikiwa zimebaki chini ya ulinzi wa jeshi la police.
Akizungumzia operesheni hiyo Kamanda wakulyamba alisema kuwa operesheni hiyo niendelevu katika wilaya zote za mkoa wa Tanga '' tunaendelea na operesheni hii kwani wananchi wamechoka na ajari za barabarani na sisi jeshi la police tumejipanga kuhakikisha tunatokomeza ajari zinazotokana na pikipiki maarufu kama bodaboda wito wangu kwa madereva na wananchi kwaujumla kila mmoja azingate wajibu wake tukifanya hivyo tutaweza kutokomeza ajari pamoja na uhalifu'' alisema kamanda Wakulyamba.
Maoni
Chapisha Maoni