Zanzibar kuwa mwenyeji wa mkutano wa tatu wa watanzania wanaoishi nje ya nchi Dayasfora

Image result for Zanzibar

Zanzibar ina tegemea  kuwa mwenyeji wa mkutano wa tatu wa watanzania wanaoishi nje ya nchi Dayasfora  unaotarajia kuanza kesho ili kufanikisha  malengo ya kuanzishwa  kitengo cha wanadayasfora hao

Akitowa taarifa kwa waandishi wa habari Waziri wa  nchi Ofisi ya raisi  na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Issa Haji Ussi Gavu amesema serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa na desturi  toka mwaka 2014 na 2015 kufanya makongamano ikiwa ni   miongoni mwa ahadi ya rais mstaafu  wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakayta Mrisho  Kikwete.

Amesema kongamano hilo litakuwa na mafanikio makubwa kwa muitikio walioonesha kwa uwezo na upeo wa kuona katika kuhakikisha watanzania hao wanaiiunga mkono nchi yao Tanzania katika kuendeleza maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.


Kongamano hilo la siku mbili  linatarajia kufanyika kesho na kufunguliwa na raisi wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dokta Ali Muhammed Shein na kufungwa na raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli.

Maoni