SERIKALI YATAKIWA KUTOA ELIMU KWA WACHIMBAJI KUEPUKA MIGOGORO NA MIGONGANO

151012123026_matumaini_ya_wachimba_mgodi__yafifia_tz_624x351_bbc_nocredit

Na Mahmoud Ahmad Kondoa
Serikali kupitia ofisi ya Madini Kanda ya Kati imetakiwa kutoa elimu  ya uchimbaji madini kwa wachimbaji wadogo wa madini ilikuondoa migongano na migogoro ambayo imekuwa ikitokea mara kwa mara pindi wachimbaji wanapovumbua maeneo ya madini na kujikuta maeneo hayo wanapewa wachimbaji wakubwa bila kujali wachimbaji waliokuwepo awali.
Kauli hiyo imetolea kwa nyakati tofauti na wachimbaji wa Dhahabu kwenye Kata ya Changaa Wilayani Kondoa walipokuwa wakijadili zuio la uchimbaji wa eneo  walilokuwa wanachimba tokea mwaka 2012 hadi suluhisho la mgogoro wao utakapopatiwa ufumbuzi kwenye ofisi za Afisa madini mkazi Dodoma na kuzitaka mamlaka kuacha kuwakumbatia wawekezaji na kuona wao ndio msingi kuliko wachimbaji wadogo waliokuwa kwenye maeneo hayo kwa mda mrefu.
 Wamesema kuwa Kabla mgogoro huo haujaanza walikuwa wakichimba eneo la namba mbili na mwekezaji huyo alikuja na kuwaondoa ambapo walisogea eneo la namba mmoja na kwa sasa amekuja tena na kutaka kuwaondoa akidai kuwa amepewa leseni na kamishna msaidizi wa madini na kuwa eneo hilo linamilikiwa na Kampuni ya Kondoa Minning (T)Ltd.
Said Ramadhani ni mmojawapo wa wachimbaji katika eneo hilo anasema kuwa kumekuwepo na sintofahamu ya hatima ya wao kuendelea na uchimbaji baada ya barua ya Kaimu Afisa madini mkazi Affa .E. Affa kuwataka kusimama kwa leseni za uchimbaji na shughuli katika eneo la kijiji cha Changaa licha la suala hilo kuwepo mezani mwao na majibu kutojibiwa kwa mda wa miezi miwili toka tar.24 mwezi wa 5 mwaka huu juu ya nani hasa ni mmiliki wa eneo hilo linalogombewa kuanzia no 1 hadi 4.
Ramadhani alisema kuwa licha ya kutuma maombi ya leseni ya umiliki wa eneo hilo wanaona wachimbaji hawatendewi haki wakiambia Kondoa minning ina leseni na wao wakiambia leseni zao zimefutwa hali inayowachanganya hadi sasa kuhusiana na sakata hilo na kuiomba serikali kuja kutoa elimu kwao kuhusiana na suala zima la madini ili waweze kuwalipa mrabaha na kodi ya serikali kwani hawana wasi wasi na ulipaji.
Nae Mwenyekiti wa Kikundi cha Kumucha  Donmillan Shirima alisema wanaheshimu maamuzi ya Afisa Madini Mkazi Dodoma na watayazingatia ila muda wa majibu yao umechukuwa mda mrefu ikizingatiwa wao wanategemea suala la uchimbaji kuendesha maisha yao ya kila siku kwani miezi miwili ni mingi nab ado majibu hayajatoka tokea zuio lilipotangazwa Tar.24 ya mwezi 5 mwaka huu.
Shirima alisema kuwa wao wamekuwa wakitii agizo hilo ila mwekezaji huyo ambaye anashirikiana na wabia kutoka nchini Kenya kwenye umiliki wa hisa za kampuni hiyo bila kufuata sheria za madini na ofisi ya madini kubariki kuwapa leseni na kuaacha maombi ya awali ya kikundi hili linatuweka kwenye njia panda kujua hatma yetu kwani suala hapa ni uvunjaji wa sheria za madini uliofanywa na Kampuni hiyo ya Kondoa Minning iliyochini ya mwavuli wa Kampuni ya Kidee Minning (T)Ltd
Wakati huo huo Kamishna wa Madini Kanda ya Kati alipotakiwa Kutoa Majibu ya Wachimbaji Hao aliliambia Gazeti hili kuwa kwa kuuliza hao wachimbaji wana chimba kisheria kwa kufuata kanuni za baruti na wanananunua wapi, ila suala hilo lipo mikononi mwa Ofisi ya Madini ya mkazi Dodoma na yeyeto anaetaka majibu awasiliane nao ilikujua majibu ya nini kinaendelea kwenye kuupatia ufumbuzi mgogoro huo.
Alipotafutwa meneja wa kampuni ya Kidee Minning ambao ndio washirika wa Kondoa Minning Ismail Kidee alisema kuwa suala hilo wao wana leseni na kweli waliwakuta wachimbaji hao kwenye eneo hilo na kuahidi kushirikiana na wachimbaji hao katika kuhakikisha wanapata haki yao kama alivyoaahidi kwenye mkutano mkuu wa Kijiji cha Changaa mwaka 2015.
Sakata la hatua ya ofisi ya Afisa madini mkazi kutoa Zuio la leseni za Uchimbaji wa Madini kwenye Kijiji cha Changaa na kuundika barua bila kuwepo muhuri limewaacha wachimbaji njia panda na kuitaka kuhakikisha suala lao linapitiwa bila kuangalia nani nacho na kuzitaka mamlaka kuwa makini na kusogea kulitazama suala hilo kwa ukaribu.
Mogogoro wa eneo hilo unaogombewa na Kikundi cha Kumucha ambapo  wachimbaji wadogo ndio wanachama wa kikundi hicho pamoja na Kampuni ya Kidee yenye Ubia na Kondoa Minning huku wengine wakiwa ni Kampuni ya Millenium Builders Ltd ambapo mvutano huo umekuwepo tangia Tar.8 mwezi wa Tatu mwaka huu baada ya uongozi wa Kijiji cha Changaa na Mtaa wa Tumbelo kuitambulisha Kondoa Minning kuwa inamiliki eneo hilo na kuwaacha wachimbaji wadogo kutojua hatma yao licha ya kuvumbua madini hayo na kutuma maombi ya kuomba leseni kutotimia.

Maoni