UMEWAHI KUONA MASHINDANO YA KUTENGENEZA KEKI?? SHUHUDIA HAPA.

Baadhi ya wananchi waliotembelea Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ wakipita kuangalia keki.
Majaji wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' watipita kukagua, kupata maelezo ya watengenezaji wa keki hizo kabla ya kuwapata washindi.
Majaji wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ watipita kukagua, kupata maelezo ya watengenezaji wa keki hizo kabla ya kuwapata washindi.
Baadhi ya wananchi waliotembelea Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' wakipita kuangalia keki.
Baadhi ya wananchi waliotembelea Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ wakipita kuangalia keki.
Marion Elias Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, ambaye pia Mratibu wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) katika maonesho hayo.
Marion Elias Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, ambaye pia Mratibu wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) katika maonesho hayo.
Majaji wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' watipita kukagua, kupata maelezo ya watengenezaji wa keki hizo kabla ya kuwapata washindi.
Majaji wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ watipita kukagua, kupata maelezo ya watengenezaji wa keki hizo kabla ya kuwapata washindi.
Majaji wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' watipita kukagua, kupata maelezo ya watengenezaji wa keki hizo kabla ya kuwapata washindi.
Majaji wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ watipita kukagua, kupata maelezo ya watengenezaji wa keki hizo kabla ya kuwapata washindi.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' katika picha ya pamoja
Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ katika picha ya pamoja
Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' katika picha ya pamoja.
Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ katika picha ya pamoja.
Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' katika picha ya pamoja.
Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ katika picha ya pamoja.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Majaji wa Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' wakijumuisha alama kabla ya kuwapata washindi.
Majaji wa Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ wakijumuisha alama kabla ya kuwapata washindi.
Baadhi ya wananchi waliotembelea Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' wakipita kuangalia keki.
Baadhi ya wananchi waliotembelea Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ wakipita kuangalia keki.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya 'Azam World of Cakes Exhibition' yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
Keki mbalimbali zilizoshiriki katika Maonesho ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’ yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.


JOPO la Majaji watatu na mabingwa wa fani za mapishi leo wamewatangaza mabingwa wa utengenezaji keki waliojitokeza katika Maonesho ya bidhaa za keki ‘Azam World of Cakes Exhibition’ yaliofanyika katika Hoteli ya Serena ya jijini Dar es Salaam.
  Jumla ya makampuni na watengenezaji keki wapatao 39 wameshiriki katika maonesho hayo ya keki yalioandaliwa na kampuni ya Insights Productions Limited kwa udhamini wa Kampuni ya Azam Tanzania.

Akitangaza washindi katika maonesho hayo ya keki, mmoja wa majaji ambaye pia ni Mpishi Mkuu, toka Ramada Encore ya jijini Dar es Salaam, Edward Mukabana alisema timu ya majaji hao imewapata washindi wa kwanza watatu katika makundi matatu; yaani mshindi wa Keki yenye Radha Bora, Mbunifu Bora wa Keki na Mshindi wa Keki yenye Mvuto Kimuonekano.

Jaji huyo wa ‘Azam World of Cakes Exhibition’ aliwataja Amina Salim kuwa ndiye aliyeibuka mshindi wa keki yenye radha bora zaidi, huku kampuni ya Beta Bakery ikitwaa taji la mbunifu Bora wa Maonesho hayo ya keki. Pia alimtangaza Janeth Muawiriro kuwa ndiye mshindi wa keki yenye Mvuto kimuonekano katika washiriki wote.

Jopo hilo la majaji wa ‘Azam World of Cakes Exhibition’ pia lilimtangaza Leila Dhiyebi kuwa ni mshindi wa kwanza aliyepigiwa kura na wananchi waliotembelea maonesho hayo makubwa ya keki Tanzania. Kundi lingine la washindi ambao keki zao ziliwavutia majaji ni pamoja na Haika Shao na Caroline Gul pamoja na wanae wawili ambao walishiriki kubuni umbo la keki kwa mchoro iliyotengenezwa na mamayao.

Akizungumza awali kabla ya kuwatangaza washindi, Jaji Mkuu wa Mashindano hayo ya ‘Azam World of Cakes Exhibition’, Tom Owino (Excetive Chef) alisema walisema wamezipitia keki zote za washiriki kuangalia vigezo mbalimbali vya upishi, muonekano na kuonja radha ya kila keki kabla ya kukaa chini na kuanza kufanya maamuzi ya pamoja ya majaji kwa kuzingatia vigenzo vya msingi katika utengenezaji keki.

Aidha kwa upande wake, Marion Elias Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, ambaye pia ni Mratibu wa maonesho hayo alisema maonesho hayo yamekuwa na mvuto baada ya kushirikisha makampuni na watu binafsi huku yakilenga kutangaza bidhaa nzima ya keki na ubunifu katika utengenezaji.

Alisema washiriki wote wamepata fursa ya kubadilishana uzoefu na kujifunza ubunifu zaidi wa shughuli hizo toka kwa wataalam wengine jambo ambalo litawabadili kwa namna fulani, ikiwa ni pamoja na kupata zawadi toka kampuni ya Azam na vyeti maalum vya kutambua mchango wao kiushiriki.

Kwa upande wake Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma toka Kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan alisema Azam ikiwa ni kampuni inayotengeneza unga bora wa kutengenezea keki imeamua kudhamini ikiwa ni ishara ya kutambua taaluma hiyo ya utengenezaji wa keki nje na ndani ya Tanzania. Wananchi walipata fursa ya kuangalia keki mbalimbali pamoja na kuonja radha zake jambo ambalo lilileta mvuto zaidi kwa washiriki.
  *Imeandaliwa na www.thehabari.com

Maoni