Wakazi wa jiji la Arusha
waimeitaka wizara ya maliasili na Utalii kuanzisha siku ya faru hapa
nchini ikuweza kuuhisha maisha ya mnyama huyo aliyehatarini kutoweka
hapa nchini huku wakiitaka Serekali kuangalia suala zima la utunzaji wa
maeneo ya hifadhi za akiba kabla ya upimaji wa vijiji .
Kauli hiyo imetolewa na Mgeni
rasmi mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyirembe Mnasa kwa niaba ya waziri wa
utalii Lazaro Nyalandu katika kilele cha ufungaji wa wiki ya Utalii
duniani kitaifa iliyofanyika katika viwanja vya maonyesho ya Nanenane
Themi jijini hapa huku akisisitiza kuangalia suala zima la ushoroba
kwani limekuwa katika migogoro na kuwafanya wanyama kukosa maeno yao ya
Asili.
Dc Mnasa alisema kuwa Rasilimali
hizo za taifa zinahitaji kupangwa katika kuangalia hali ya kuinufaisha
jamii yote kwani sekta ya utalii imekuwa ikisaidia kupunguza wimbi la
ukosefu wa ajira hapa nchini na kuwataka jamii iliyopembezoni na hifadhi
kuendelea kutunza uikolojia na kuacha uchafuzi wa mazingira
yanooizunguka kwa vizazi vya wanyama na faida kwa jamii.
Aliitaka jamii hasa wakazi wa
jiji la Arusha kupenda vivutio vya utalii ikiwemo kuvitembelea na pia
kujifunza kwani itasaidia kuwapatia ajira kwa kuweza kuwaelekeza wageni
wanaotembelea hapa mkoani Arusha kwa shughuli za kiutalii kama sheria ya
mwaka 2008 ilivyoainisha juu ya utalii wa ndani.
“Tuendelee kujifunza na tunaomba
wananchi wote waliokaribu na hifadhi za taifa kukabiliana na changamoto
ya vita dhidi ya ujangili inayoendelea kote nchini ikiwemo ya tembo na
Faru wanyama waliohatarini kutoweka,pia upimaji wa vijiji ukaendana na
mazingira ya uikoloia ilikuweza kuweka mapitio ya wanyama”alisema Mnasa
Nae Mkurugenzi wa Bodi ya utalii
hapa nchini Zahoro Kimwaga alisema Mnyama faru wapo 92 hapa nchini
hivyo ni mnyama pia alie hatarini kutoweka akawataka vijana kuanza
mapambano ya kuhakikisha kuwa mnyama huyo analindwa kwa gharama yeyote
ikiwemo kuweka maadhimio yatakayosaidia utunzaji wa wanyama hao.
Kimwaga alisema kuwa Tembo leo
hawezi kuishi nje ya hifadhi zetu kama hapo awali sababu kubwa ni
ujangili hivyo na wasihii wananchi kutoa taarifa pindi wanapoona hujuma
dhidi ya wanayamapori kwenye maeneo yao.
Alisema kuwa mapambano haya
yanihitaji mashirikiano kwani jamii inayofanya matukio ya kiuhalifu
hususasni ujangili tunaishi nayo na kuijua hivyo mchango wa wananchi
kwenye vita ya ujangili una sehemu yake katika kufanikisha vita hiyo.
“Msisahau kutembelea na
kuhamasisha utalii wa ndani utsaidie kuijenga nchi yetu pia suala la
kujifunza ni msingi kwa wakazi wa maeneo yanaozunguka hifadhi zetu kwa
ni ajira tosha,pia msiasahau utalii wa kiutamaduni kwani umekuwa
ukishika kasi kwa sasa”alisema kimwaga.
Maoni
Chapisha Maoni