Hapo awali waziri mkuu wa Lesotho, Tom Thabane, aliiambia BBC ameondoka Lesotho baada ya kutishwa kuwa atauwawa.
Aliongeza kusema kuwa hatua za jeshi zimeifanya serikali isiweze kufanya kazi, na ni sawa na mapinduzi.
Lakini jeshi la Lesotho limekanusha kuwa limejaribu kupindua serikali.
Mwandishi wa BBC mjini Johannesburg anasema hali sasa imekuwa shuwari katika mji mkuu, Maseru.
Lesotho ni nchi iliyozungukwa kabisa na Afrika Kusini na inaitegemea sana Afrika Kusini kwa ajira na pato
Maoni
Chapisha Maoni